emblem

The United Republic of Tanzania

National Social Security Fund (NSSF)

We Build Your Future

News

MWENYEKITI WA BODI YA WADHAMINI YA NSSF, ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA NSSF


Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya NSSF, Bi. Mwamini Malemi, ametembelea Makao Makuu ya NSSF jijini Dar es Salaam, leo tarehe 5 Disemba 2023, na kuzungumza na Menejimenti ya Mfuko, ambapo amepata nafasi ya kupokea taarifa ya utendaji kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba, ambaye alitumia fursa hiyo pia kumpongeza na kuahidi kumpatia ushirikiano mkubwa katika utekelezaji wa majukumu yake pamoja na Bodi ya Wadhamini kwa ujumla.