News
NSSF YATATUA KERO ZA WANACHAMA
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Rukwa, Daudi Mhongole (kushoto) akimuhudumia mwanachama aliyetembelea banda la NSSF wakati wa maonesho ya kilimo na biashara yanayofanyika katika viwanja vya Nelson Mandela Mkoani Rukwa.
NSSF inatumia maonesho hayo kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa sekta binafsi na sekta isiyo rasmi, matumizi ya mifumo ya TEHAMA kwa mwanachama na mwajiri ili kumrahisishia huduma bila kulazimika kufika katika ofisi za NSSF, kusikiliza na kutatua kero za wanachama na kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji ikiwemo miradi ya nyumba za kisasa na viwanja.

