News
TUNAWASHUKURU WANANCHI WA MKOA WA ARUSHA KWA KUAMUA KUWA MASTAA WA MCHEZO WA NSSF

NSSF tunawashukuru sana Wananchi Waliojiajiri katika Jiji la Arusha kwa kuchangamkia fursa hii ya kuwa Mastaa wa Mchezo wa NSSF kwa kuamua kujiunga na kuchangia katika Mfuko ili kujiwekea akiba kwa ajili ya kesho iliyokuwa njema na hatimaye wanufaike na mafao yanayotolewa yakiwemo ya matibabu.
Kujiunga na kuwa Staa wa Mchezo wa NSSF ni rahisi sana kwani unatakiwa kubofya *152*00# kisha fuata maelekezo. Tunawakaribisha Mastaa wa Mchezo wafike hapa Soko la Kilombero jijini Arusha, wanufaike na elimu ya hifadhi ya jamii kwa Wananchi Waliojiajiri.
NSSF STAA WA MCHEZO, HIFADHI SCHEME - HIFADHI YA JAMII KWA WOTE